Powered By Blogger

11.12.17

Arsenal yaanza kupataa makombora ya Sweden europa league

     dulahots. blogspot. com
Arsenal imepangwa kucheza dhidi ya timu ya Ostersunds ya nchini Sweden katika Hatua ya 32 Bora ya michuano ya Europa League. 

Arsenal itawavaa wapinzani wao hao ambao wanafundishwa na Graham Potter ambaye ni raia wa Uingereza. 

Atletico Madrid wao wamepangwa kukutana na Copenhagen wakati Borussia Dortmund itakutana na wabishi kutoka Italia, Atalanta ambao waliifunga Everton nyumbani na ugenini katika hatua ya makundi ya michuano hiyo. 

Makocha wawili waliowahi kufanya kazi England wanatarajia kukutana pia katika hatua hiyo wakati ambapo Celtic inayonolewa na Brendan Rodgers itakutana na Zenit St Petersburg iliyochini ya Roberto Mancini. 

Kocha Gennaro Gattuso wa AC Milan ataiongoza timu yake hiyo kuivaaa Ludugorets ya Bulgaria. 

Ratiba kamili inaonyesha hatua hiyo itachezwa Februari 15 wakati mechi za marudio ni Februari 22, mwakani 2018. 

RATIBA KAMILI YA 32  
Borussia Dortmund vs Atalanta 

Nice vs Lokomotiv Moscow 

Copenhagen vs Atletico Madrid 

Spartak Moscow vs Athletic Bilbao 

AEK Athens vs Dynamo Kiev 

Celtic vs Zenit St Petersburg 

Napoli vs Leipzig 

Red Star Belgrade vs CSKA Moscow 

Lyon vs Villarreal 

Real Sociedad vs Salzbug 

Partizan Belgrade vs Viktoria Plzen 

Steaua Bucharest vs Lazio 

Ludogorets vs AC Milan 

Astana vs Sporting Lisbon 

Ostersunds vs Arsenal 

Marseille vs Braga 

No comments:

Post a Comment

Kocha boraa Mara nne mfululizoooo EPL gurdiola

         @dullahots.blogspot.com Kocha wa Manchester City, Pep Guardiola ameweka rekodi ya kuwa kocha wa kwanza kutwaa tuzo ya kocha bo...